Tuesday, May 17, 2011

CHUO KIKUU CHA DODOMA
SERENGETI SOCIETY OF UDOM (SSUDOM)
KANUNI ZA KIKUNDI KWA MWAKA 2010/2011

Kwa ajili ya kutoa tafsiri ya baadhi ya vifungu vya katiba ya SSUDOM, kanuni hizi zimetolewa ili kuendesha shughuli za kikundi kwa mwaka wa masomo 2010/2011

  1. Kila mwanachama atatakiwa kulipa kiingilio (Entrance fees) cha TSH 10,000/=
  2. Kila mwanachama atatakiwa kulipa Kiasi cha  TSH 5,000/= kwa kila mhula isipokuwa kwa mhula aliolipia kiingilio.
  3. Kila mwanachama atatakiwa kutoa mchango wa TSH 3,000/= kwa ajili ya faraja au pongezi kwa mwanachama anayestahili kupewa kwa wakati huo.
  4. Kikundi kitatoa kiasi kitakachosalia kufika shilingi laki moja (100,000/=) kwa ajili ya faraja au pongezi kwa mwanachama anayestahili kwa wakati huo.
  5. Mkopo usiozidi shilingi laki moja (100,000/=) utatolewa kwa mwanachama atakayehitaji kufanya hivyo kulingana na mfuko wa chama.
  6. Mkopo kwa mwanachama hautakuwa na riba, ila mkopaji atatakiwa kulipa asilimia kumi (10%) kwa ajili ya gharama za kupata huduma za kibenki.
  7. Mwanachama atatakiwa kurudisha Kiasi cha fedha alichokopa kwa muda usiozidi miezi miwili.
  8. Mwanachama anayehitaji mkopo asiwe anadaiwa na kikundi wakati mkopo unapoombwa.
  9. Mapato na matumizi ya kikundi yatasomwa katika mkutano mkuu wa kila mwisho wa muhula.








NB Pesa ikishalipwa haitarejeshwa. 

No comments:

Post a Comment